Chuo Kikuu cha Witwatersrand
From Wikipedia, the free encyclopedia
Chuo Kikuu cha Witwatersrand | |
---|---|
Staff | 1 951 |
Wanafunzi | 24 381 |
Mahali | {{{mji}}} |
Tovuti | http://www.wits.ac.za/ |
Chuo Kikuu cha Witwatersrand, Johannesburg ni mojawapo ya vyuo vikuu bora vya Afrika Kusini lililoko katika maeneo ya kaskazini ya katikati mwa Johannesburg. Kinajulikana vizuri zaidi kama Wits University. Chuo hiki kina mizizi yake katika sekta ya madini, kama ilivyo Johannesburg na Witwatersrand kwa ujumla.
Mwaka wa 1959, sheria ya Extension of Education Act iliweka vikwazo kwa usajili wa wanafunzi weusi kwa karibu kipindi chote cha sera ya kibaguzi; hata hivyo, viongozi kadhaa weusi mashuhuri walihitimu kutoka chuo hiki. Kilimaliza ubaguzi tena punde tu kabla ya kukomeshwa kwa sera ya kibaguzi ya apartheid mwaka wa 1990. Baadhi ya wakosoaji wengi wa enzi ya kibaguzi, wa aidha asili ya kizungu au Kiafrika, walikuwa wakati moja wanafunzi na wahitimu wa chuo hiki.