Mikolojia
From Wikipedia, the free encyclopedia
Mikolojia ni tawi la biolojia linalohusika na uchunguzi wa kuvu, ikiwa ni pamoja na maumbile na biokemia, uainishaji wao na matumizi yao kwa binadamu kama chanzo cha tinder, dawa na chakula, pamoja na hatari zao, kama vile sumu au maambukizi. Kuvu wengi wanazaa sumu, dawa na metaboliti, kwa mfano, aina fulani ya Fusarium.
Mtu anayesomea au profesa wa mikolojia anajulikana kama mwanamikolojia. Baadhi ya wanamikolojia ni kama vile: Elias Magnus Fries, Christian Hendrik Persoon, Anton de Bary na Lewis David von Schweinitz. Maneno "mikolojia" na "mwanamikolojia" yalianza kutumika mwaka 1836 na M.J. Berkeley.
Kihistoria, mikolojia ilikuwa tawi la botania kwa sababu, ingawa kuvu ni mageuzi ya karibu sana na wanyama kuliko mimea.