Benedikto Mwafrika
From Wikipedia, the free encyclopedia
Benedikto Mwafrika (San Fratello, wilaya ya Messina, mkoa wa Sisilia, Italia, takriban 1524 - Palermo, 4 Aprili 1589) alikuwa bradha Mfransisko maarufu kwa unyenyekevu na imani katika maongozi ya Mungu.
Kutokana na sifa yake, mwaka 1652 aliteuliwa na Bunge la Palermo kuwa mmojawapo kati ya wasimamizi wa jiji hilo. Tarehe 15 Mei mwaka 1743 Papa Benedikto XIV alimtangaza mwenye heri, halafu Papa Pius VII alimtangaza mtakatifu tarehe 24 Mei 1807, akiwa Mnegro wa kwanza kutangazwa na Kanisa Katoliki kuwa hivyo.
Anaheshimiwa kama msimamizi wa Waafrika, hasa Amerika Kusini.