Krim
From Wikipedia, the free encyclopedia
Krim (kwa Kirusi Крым Krym; kwa Kiukraina Крим Krim; kwa Kitartari Qırım; kwa Kiingereza Crimea) ni rasi upande wa kaskazini wa Bahari Nyeusi yenye eneo la km² 26.100.
Kisiasa ni jimbo la kujitawala ndani ya nchi ya Ukraine na jina rasmi ni "Jamhuri ya kujitawala ya Krim". Tangu mwaka 2014 ilivamiwa na kutekwa na jeshi la Urusi na kutangazwa kuwa sehemu ya Urusi, hatua isiyotambuliwa na umma wa kimataifa. Zaidi ya nusu ya wakazi 1.994.300 (mwaka 2005) ni Warusi (58,5 %), takriban robo Waukraine (24,4 %) halafu kuna pia Watartari 243.400 (12,1 %).