Maunzingumu
ukarasa wa maana wa Wikimedia / From Wikipedia, the free encyclopedia
Maunzingumu (pia maunzi ngumu[1]; kwa Kiingereza: hardware) ni sehemu za kompyuta zinazoshikika . Maunzingumu ni vifaa mbalimbali vinavyounda mashine ya kompyuta, navyo vimegawanyika katika sehemu kuu tatu:
- vifaa vya kuingizia data (Input devices),
- vifaa vya kutolea data (Output devices) na
- vifaa katika tarakilishi (Kadi ya mtandao, Kadi ya sauti, diski kuu).
Maunzingumu haina kazi bila programu na data za maunzilaini.