![cover image](https://wikiwandv2-19431.kxcdn.com/_next/image?url=https://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/d/df/Jadwiga_Jan_Matejko_%2528Poczet%2529.jpg/640px-Jadwiga_Jan_Matejko_%2528Poczet%2529.jpg&w=640&q=50)
Hedwiga wa Poland
From Wikipedia, the free encyclopedia
Hedwiga (kwa Kijerumani Hedwig; kwa Kipolandi Jadwiga, linatamkwa jadˈviɡa; Budapest, Hungaria, 1373/1374 - Krakov, Polandi, 17 Julai 1399) alikuwa malkia wa Polandi na Lituania.
![Thumb image](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/d/df/Jadwiga_Jan_Matejko_%28Poczet%29.jpg/320px-Jadwiga_Jan_Matejko_%28Poczet%29.jpg)
![Thumb image](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/2/2c/Coat_of_arms_of_Jadwiga_of_Poland.svg/640px-Coat_of_arms_of_Jadwiga_of_Poland.svg.png)
Kuanzia mwaka 1384 hadi kifo chake alitawala nchi ya Poland akiitwa 'mfalme' badala ya 'malkia', ili kusisitiza kwamba hakuwa tu mke wa mtawala halisi[1].
Alizaliwa katika ukoo wa Wakapeti wa Anjou, binti wa mwisho wa mfalme Luis I wa Hungaria na Elizabeti wa Bosnia.[2].
Kwa kuolewa na Ladislaus wa Lituania, alimfanya abatizwe akaeneza Ukristo katika nchi hiyo ya Kipagani [3].
Tangu zamani anaheshimiwa na Kanisa Katoliki kama mtakatifu na msimamizi wa kila malkia. Papa Yohane Paulo II ndiye aliyemtangaza rasmi mwenye heri tarehe 8 Agosti 1986 na mtakatifu tarehe 8 Juni 1997.